Monday 4 April 2016

Sheria ya Mtoto ya Mwaka 2009.

ad300
Advertisement

1.Utangulizi

Kabla ya kutungwa kwa Sheria ya Mtoto ya Mwaka 2009 maswala ya mtoto nchini  Tanzania yalikuwa yameunganishwa katika Sheria ya Malezi,(Sura ya 278),Sheria ya kuasili Mtoto(Sura ya 335), Sheria ya Udhibiti wa Nyumba za Watoto (Sura ya 61), na Sheria nyingine. Hali hii ilisababisha ugumu katika uelimishaji na  utekelezaji wa masharti husika.

Mnamo mwaka 2009 Serikali iliamua kutunga Sheria mpya ya Mtoto kwa lengo la kuunganisha masharti husika katika sheria moja  na kuyaboresha zaidi kulingana na  mazingira yetu.
Hali halisi ya kijamii na kiuchumi pamoja na Mikataba ya kimataifa ambayo  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  imesaini na kuridhia  ikiwemo Mkataba wa  Umoja wa Mataifa wa Haki za  Mtoto, pamoja na hitifaki zake za nyongeza na Mkataba wa Haki na Ustawi wa Mtoto wa Afrika.

Sheria ya Mtoto ya mwaka 2009 ilipitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  tarehe 4 Novemba,2009 na kusainiwa na Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (mstaafu awamu ya nne)  tarehe 20 Novemba,2009.
Sheria hii imechapishwa katika gazeti la  Serikali  Namba 156 na kuanza kutekelezwa tarehe 16 Aprili,2010.

2.Madhumuni
Sheria ya Mtoto  Na.21 ya mwaka 2009  ina madhumuni yafuatayo:-
1. Kurekebisha na kuweka  pamoja masuala ya mtoto katika sheria moja ya Mtoto.

2. Kuweka masharti maalum kwa  ajili ya kuendeleza ,kuboresha,kuhifadhi na kulinda Haki za Mtoto zilizoainishwa katika sheria mbalimbali ili kukidhi matakwa ya Mikataba ya Kimataifa na Kikanda kuhusu Haki na Ustawi  wa mtoto tuliyoisaini na kuridhia. Hii ni pamoja na Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Mtoto ya mwaka 2008.

3. Kuweka masharti yanayoondoa ubaguzi kwa mtoto pamoja na ubaguzi wa kijinsia, dini, ulemavu na Siasa.

4. Kulinda na kuhifadhi haki za mtoto na kutoa tafsiri ya neno "Mtoto" ambalo  litatumika sambamba na  tafsiri  katika Sheria zote za nchini, Katiba ya Nchi, Mikataba ya Kimataifa na sera ya Taifa ya Maendeleo ya mtoto ya mwaka 2008.

5. Kuanisha Haki za mtoto kwa kuzingatia misingi ya Ustawi, haki ya Kuishi na wazazi wake, kudhibiti vitendo vitokanavyo  na  mila zinazoleta madhara ,kuzuia na kudhibiti ajira hatarishi kwa watoto  kwa kuzingatia watoto wenye mahitaji maalum.

6. Kuweka mazingira yatakayoongoza  taratibu  za matunzo kwa mtoto kwa kuzingatia gharama za maisha , sehemu husika na hali halisi ya  kiuchumi pamoja na uwezo wa wazazi.

7. Kuweka masharti yanayohusu watoto walio katika ukinzani na  sheria kwa kuainisha utaratibu wa kumshughulikia mtoto na kutoa adhabu mbadala ya kifungo  kwa lengo la kumrekebisha na kuweka masharti ya kuasili mtoto.

Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: