Sunday 2 April 2017

Autism/ Usonji

ad300
Advertisement

Ugonjwa wa Usonji kwa lugha ya kiingereza ni Autism, ni ugonjwa ambao kwa mujibu wa shirika la afya duniani, WHO  hukumba mtoto mmoja kati ya kila watoto 160 duniani. Usonji ni tatizo la kibaiolojia analopata mtoto anapokuwa tumboni mwa mama yake na dalili huonekana kuanzia umri wa miaka mitatu na kuendelea.Kabla ya hapo wataalamu wanasema ni aghalabu kuona dalili hizo ambapo zinapojitokeza mtoto hukosa mbinu za uhusiano, anashindwa kuzungumza na wakati mwingine kurukaruka na hata kujing'ata. Watoto hawa kutokana na tatizo hilo wengine hutekelezwa na jamii na kunyimwa haki zao za msingi ikiwemo kuishi, kuendelezwa, kulindwa na kushirikishwa. Hata hivyo katika siku ya kimataifa ya usonji duniani tarehe Pili Aprili Umoja wa Mataifa umetaka elimu zaidi ili jamii ibadili mtazamo kwani watoto wenye usonji wakipatiwa huduma mapema wanaweza kushiriki vyema katika jamii zao kwani wana uelewa wa hali  ya juu. Nchini Tanzania harakati za kuelimisha jamii kuhusu Usonji zilikwishaanza.

#Sambaza #share #autism #usonji #tanzania #sdgs

Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: