Thursday 6 October 2016

Uchaguzi Baraza La Watoto Moshi

ad300
Advertisement

September  26th, 2016 Watoto kutoka katika viunga mbalimbali vinavyounda Halmashauri  ya Wilaya  ya Moshi walikusanyika kwa pamoja katika Ofisi za Halmashauri  hiyo maarufu kama "KDS" kuwawakilisha watoto wenzao ambao hawakuweza kupata fursa hiyo.

Lengo na dhumuni la mkutano huo ilikuwa ni Uchaguzi  Mkuu wa kupata baraza jipya  la  Watoto  Halmashauri  ya Wilaya  ya Moshi kama ulivyo utaratibu wa mabaraza ya Watoto nchini Tanzania  uchaguzi  Mkuu wa Mabaraza  ya  Watoto  hufanyika kila baada ya miaka miwili, wale ambao umri wa  miaka 18 hawataruhusiwa tena kugombea nafasi yoyote ndani ya Baraza hilo hila baadhi ya viongozi waliovuka umri wa miaka 18 wanapata nafasi ya kuwa Washauri wa Baraza husika,kama ilivyofanyika kwa Baraza  la Watoto  Halmashauri  ya Wilaya   Moshi  Mwenyekiti ambae amemaliza muda wake ndg Mohamed R. Gea na aliyekuwa Makamu Mwenyekiti  wa Baraza  hilo ndg Peniel Mlay watakuwa washauri  wa Baraza hilo ambalo litaongozwa chini ya Mwenyekiti  mpya ndg Kingslay Sama.

Baraza la Watoto  ni chombo huru kilichoundwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano Watanzania  ili kiwezesha maslahi bora ya mtoto nchini yanalindwa na watoto  wenyewe wanapata nafasi ama chombo cha kuwawakilisha.

Kauli Mbiu ya Baraza la watoto ni:- "KULINDA NA KUTETEA HAKI ZA MTOTO NI JUKUMU LANGU MIMI NA WEWE"

Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: